Tuesday, March 24, 2015

FA YAJIPANGA KUBORESHA TIMU YA TAIFA KWA KUPUNGUZA WACHEZAJI WA NJE.

SHIRIKISHO la Soka la Uingereza-FA linakusudia kuandaa sheria itakayopunguza idadi ya wachezaji kutoka nje ya nchi za umoja wa Ulaya kusajiliwa katika ligi ya nchi hiyo. Mwenyekiti wa FA Greg Dyke amesema Ligi Kuu iko kwenye hatari ya kutowasaidia wachezaji wazawa kama hatua za makusudi na haraka hazitachukuliwa kusaidia suala hilo. Katika mpango huo FA pia itaweka sheria ngumu kwa wachezaji wenye vipaji waliokulia nchini humo. Mikakati hiyo yote ina dhumuni la kuimarisha timu ya taifa ya Uingereza ambayo imekuwa haifanyi vizuri kwenye mashindano ya kimataifa.

No comments:

Post a Comment