Tuesday, March 24, 2015

KLOSE KUGEUKIA UKOCHA AKITUNDIKA DARUGA ZAKE.

MSHAMBULIAJI wa zamani wa kimataifa wa Ujerumani, Miroslav Klose ana mipango ya kuja kuwa kocha pindi atakapotundika daruga zake rasmi huku akipendelea zaidi kufanya kazi nchini kwao katika Bundesliga. Akihojiwa Klose ambaye alistaafu soka la kimataifa baada ya michuano ya Kombe la Dunia nchini Brazil, amesema malengo yake ni kuja kuwa kocha wa Bundesliga. Nyota huyo aliendelea kudai kuwa pindi atakapokuwa akitafuta leseni ya ukocha atafanya bidii zote kama anavyofanya katika mambo yake mengi. Klose mwenye umri wa miaka 36 ambaye kwasasa anacheza katika klabu ya Lazio ya Italia, aliweka rekodi katika Kombe la Dunia kwa kuwa mchezaji aliyefunga mabao mengi zaidi katika michuano hiyo akiwa mabao 16. Nyota huyo alifikisha bao la 16 baada ya kufunga bao katika mchezo ambao Ujerumani uliwashindilia bila huruma wenyewe wa michuano hiyo Brazil kwa mabao 7-1.

No comments:

Post a Comment