Monday, March 30, 2015

NEWCASTLE YATANGAZA KUINGIZA FAIDA.

KLABU ya Newcastle United imetangaza kuweka rekodi kwa mapato ya mwaka baada ya kuingiza kiasi cha paundi milioni 18.7, ukiwa ni mwaka wan ne mfululizo kutengeneza faida. Hata hivyo deni la klabu hiyo limeendelea kubakia vilevile paundi milioni 129, ukiwa ni mkopo kutoka kwa mmiliki wake Mike Ashley. Mkurugenzi mtendaji wa klabu hiyo Lee Charnley amesema faida inayopata klabu hiyo inatokana na kuungwa mkono na Ashley kwani kunawapa uimara ambao unawasaidia kukua ndani na nje ya uwanja. Charnley amesema matokeo hayo yanamaanisha kuwa wanasonga mbele kwani wana uwezo wa kutumia kiasi kwa ajili ya kuimarisha kikosi na kiasi kingine kwenda katika maeneo mengine ya biashara.

No comments:

Post a Comment