Tuesday, April 28, 2015

BAADA YA KAMPUNI YA SIMU, ETO'O SASA AHAMIA KWENYE MAVAZI.

BAADA ya kuanzisha kampuni ya siku za mkononi inayojulikana kama Eto’o Telecom nyumbani kwao, nyota wa zamani wa Cameroon Samuel Eto’o sasa anatarajia kuhamia katika ulimwengu wa mavazi kwa kuzindua nguo mbalimbali zenye nembo yake. Mojawapo ya mavazi yanayotarajiwa kutolewa kea nembo yake mpya ya Samuel Eto’o 9 ikimaanisha jezi ambayo amekuwa akivaa uwanjani, in pamoja na mashati, kofia na viatu. Kwa mujibu wa mbunifu kutoka Cameroon ambaye amebuni mpango huo, Gabriel Pascal Nyemeg Nlend amesema lengo kuu in kutambulisha mafanikio ya Samuel Eto’o katika soka la Afrika. Nlend aliendelea kudai kuwa baada ya kumaliza kazi yake uwanjani sasa wanataka Eto’o kuwasindikiza majumbani, mijini na vijijini kea kuvaa nguo zenye nembo yake. Eto’o na Nlend wanatarajia kukutana nchini Ureno baadae mwezi huu ili kukamilisha mpango huo kwabla ya kuanza kuzindua rasmi nembo hiyo katika nchi za Hispania, Urusi, Ureno na Uingereza.

No comments:

Post a Comment