Tuesday, April 28, 2015

BOURNEMOUTH, WATFORD ZAKWEA LIGI KUU UINGEREZA.

MWENYEKITI wa klabu ya Bournemouth, Jeff Mostyn amedai kuwa timu hiyo imepata mafanikio yasiwezekana baada ya kujihakikishia nafasi ya kucheza katika Ligi Kuu Uingereza msimu ujao. Mwaka 2008 klabu hiyo ilibakiza dakika tano kufilisiwa kabla ya Mostyn kutoa kitita cha paundi 100,000 kuikoa klabu hiyo. Akihojiwa Mostyn amesema klabu hiyo imepitia mambo mengi ambayo mengine yalikuwa kama hayawezekani lakini wamefanikiwa. Mwenyekiti huyo aliendelea kudai kuwa kutokana uzoefu huo anaamini wataweza kuhimili mikikimikiki ya Ligi Kuu.

No comments:

Post a Comment