Tuesday, April 28, 2015

BAADA YA KUKOSA WALICHOHITAJI KWA BALOTELLI, LIVERPOOL SASA YAMNYEMELEA JOVETIC.

KLABU ya Liverpool imeonyesha nia ya kutaka kumsajili mshambuliaji wa Manchester City Stevan Jovetic katika kipindi cha majira ya kiangazi. Kikosi hicho cha Brendan Rodgers kimekuwa na mapungufu katika safu ya ushambuliaji msimu huu hivyo kuamua kuongeza ngumu katika upande mapema pindi dirisha la usajili litakapofunguliwa. Mshambuliaji alitegemewa kuokoa jahazi Mario balotelli ambaye alisajiliwa katika dakika za mwisho katika saujili wa mwaka jana ameshindwa kuonyesha cheche zake akiwa amefunga bao moja pekee katika Ligi Kuu toka atue Anfield. City wanadaiwa kuwa tayari kumuuza Jovetic katika majira ya kiangazi lakini wangependelea zaidi mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 kwenda Serie A huku Sampdoria wakitajwa kuweza kumchukua.

No comments:

Post a Comment