Monday, April 20, 2015

BALE KUIKOSA ATLETICO MADRID.

KLABU ya Real Madrid inatarajia kumkosa winga wake mahiri Gareth Bale katika mchezo wa maruadiano wa robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Atletico Madrid kesho kutwa. Bale alipata majeruhi ambayo yalimfanya kutolewa nje katika mchezo wa La Liga ambao Madrid ilishinda mabao 3-1 dhidi ya Malaga Jumamosi iliyopita na alitegemewa kuwa nje ya uwanja kwa takribani wiki tatu. Katika taarifa yake klabu hiyo ilithibitisha taarifa za majeruhi ya mchezaji na kwamba ataukosa mchezo huo wa kesho kutwa pamoja na mingine kadhaa wakati akiendelea kupona. Madrid itaingia katika mchezo huo marudiano utakaofanyika katika Uwanja wa Santiago Bernabeu ikitafuta ushindi baada ya kutoka sare ya bila ya kufungana na majirani zao hao katika mchezo wa kwanza.

No comments:

Post a Comment