Monday, April 20, 2015

INIESTA RUKSA KUIVAA PSG KESHO.

KIUNGO wa klabu ya Barcelona Andres Iniesta amepewa ruhusa ya kucheza katika mchezo wa maruadiano war obo fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Paris saint-Germain utakaofanyika kesho. Nyota huyo wa kimataifa wa Uholanzi aliumia mgongoni wakati wa ushindi wa mabao 3-1 katika mchezo wa mkondo wa kwanza uliofanyika jijini Paris wiki iliyopita na kumfanya kuukosa mchezo wa Jumamosi iliyopita wa La Liga ambao waliwafunga Valencia mabao 2-0. Katika taarifa yake klabu hiyo ilithibitisha taarifa hizo za Iniesta kuruhusiwa kucheza katika mchezo wa kesho. Taarifa hiyo iliendelea kudai kuwa sasa itakuwa ni jukumu la meneja Luis Enrique kuamua kumtumia mchezaji huyo au la katika mchezo hu marudiano wakitafuta tiketi ya kutinga nusu fainali.

No comments:

Post a Comment