Tuesday, April 21, 2015

HAKUNA KITAKACHOWAZUIA URUSI KUANDAA KOMBE LA DUNIA LA KIHISTORIA.

RAIS wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA, Sepp Blatter amesema hakuna kitakachowazuia Urusi kuandaa michuano ya kihistoria ya Kombe la Dunia mwaka 2018. Kauli hiyo ya Blatter ameitoa wakati alipotembelea moja ya viwanja vinavyotarajiwa kutumika kea ajili ya michuano hiyo uliopo jijini Sochi. Blatter amesema anajivunia kuona Urusi ikijiandaa tayari kuwa mwenyeji wa Kombe la Dunia na hayo yote yanafanyika kwasababu ya rais wan chi hiyo Vladimir Putin. Blatter amesema michuano hiyo itakuwa ya 10 kwake baada ya kufanya kazi kea zaidi ya miaka 40 na shirikisho hilo na anategemea kuwa fainali za kipekee. Rais huyo pia aliwashukuru waziri wa michezo wan chi hiyo Vitaly Mutko na Ofisa Mkuu wa Kamati ya Maandalizi Alexei Sorokin kea ushirikiano wa hali wanaoonyesha kuhakikisha wanafanikisha tukio hilo adhimu.

No comments:

Post a Comment