Thursday, April 23, 2015

BAYERN NAO WAMNYEMELEA IVANOVIC WA CHELSEA.

KLABU ya Bayern Munich iko tayari kuongeza nguvu zake kea ajili ya kumuiba Branislav Ivanovic kutoka Chelsea katika majira ya kiangazi. Beki huyo wa kimataifa wa Serbia amebakisha mkataba wa mwaka mmoja Stamford Bridge na mabingwa hao wa Bundesliga wameungana na Paris Saint-Germain kufuatilia maendeleo ya mustabali wa mchezaji huyo kea karibu. Ivanovic amepewa ofa ya kuongezwa mkataba wa mwaka mmoja kama sera za timu hiyo zinavyotaka kwa wachezaji waliozidi umri wa miaka 30 lakini bado hajakubali kusaini. Beki huyo amekuwa tegemeo kea Chelsea toka alipojiunga nao kea kitita cha paundi milioni 9.5 akitokea klabu ya Lokomotiv Moscow ya Urusi mwaka 2008.

No comments:

Post a Comment