Thursday, April 30, 2015

CHELSEA KUTANGAZA UBINGWA MBELE YA CRYSTAL PALACE?

KLABU ya Chelsea imebakisha mchezo mmoja wa ushindi ili waweze kutawadhwa mabingwa wapya wa Ligi Kuu baada ya kutoka nyuma na kuichapa Leicester City jana katika Uwanja wa King Power. Kikosi hicho cha Jose Mourinho kililazimika kutumia mbinu zake zote kuhakikisha wanashinda katika mchezo huo mgumu dhidi ya Lecister. Ushindi huo sasa unaifanya Chelsea kukabikiwa na mechi moja ya ushindi na kama wakifanikiwa kuifunga Crystal palace katika mchezo wao utakaofanyika katika Uwanja wa Samford Bridge Jumapili hii watakuwa mabingwa rasmi wa Uingereza. Chelsea ilikuwa watangazwe mabingwa jana lakini sare ya bila kufungana dhidi ya Arsenal katika Uwanja wa Emirates Jumapili iliyopita ilikwamisha sherehe zao hizo.

No comments:

Post a Comment