Tuesday, April 28, 2015

FERGUSON AVUNJA UKIMYA NA KUDAI RONALDO NI BORA MESSI.

MENEJA wa zamani wa klabu ya Manchester United, Sir Alex Ferguson anaamini Cristiano Ronaldo in mchezaji bora wa jumla kuliko Lionel Messi. Ronaldo na Messi wameshakubalika kea kipindi kirefu kuwa wachezaji bora duniani wakiwa wamepokezana tuzo ya Ballon d’Or katika kipindi cha miaka saba iliyopita. Ferguson amewahi kumfundisha Ronaldo wakati wakiwa wote United na kocha huyo mkongwe mwenye umri wa miaka 73 anafafanua kwanini anaona Ronaldo in bora kuliko Messi. Ferguson amesema watu wanadai Messi ndio bora kuliko Ronaldo lakini hilo kea maoni yake sio kweli kwani Ronaldo anaweza kucheza kea kiwango cha hata ukimpeleka timu za daraja la chini jambo ambalo anadhani kea Messi halitawezekana. Kocha huyo aliendelea kudai kuwa Ronaldo anatumia miguu miwili, ana kasi, mzuri kea mipira ya juu na jasiri lakini Messi anadhani in mchezaji wa Barcelona pekee na sio timu zingine.

No comments:

Post a Comment