Monday, April 20, 2015

KANE ANAPASWA KUWANUNULIWA WENZAKE MSOSI - POCHETTINHO.

MENEJA wa klabu ya Tottenham Hotspurs, Mauricio Pochettino ametania kuwa Harry Kane anapaswa kuwanunuliwa wachezaji wenzake chakula cha usiku baada ya kufikisha mabao 30 msimu huu. Kane mwenye umri wa miaka 21 amekuwa mchezaji wa kwanza wa Spurs kufikisha idadi hiyo ya mabao toka mshambuliaji Gary Lineker alipofanya hivyo katika msimu wa mwaka 1991-1992. Pochettino alimpongeza Kane na kudai kuwa anastahili hatua hiyo na kutania kuwa anapswa kuwanunulia wachezaji wenzake chakula kwasababu wamekuwa wakifanya jitahada kumsaidia kufunga mabao. Akihojiwa mwenyewe Kane amesema kufikia idadi hiyo ya mabao ni jambo zuri na amewashukuru wachezaji wote kwa ushirikiano wanaompa.

No comments:

Post a Comment