Tuesday, April 28, 2015

KOCHA WA BARCELONA CHUKUA TAHADHARI KWA KUWAPUMZISHA NYOTA WAKE.

MENEJA wa Barcelona, Luis Enrique ameamua kuwaacha Gerard Pique na Thomas Vermaelen katika kikosi chake kea ajili ya mchezo wa La Liga dhidi ya Getafe. Pique amekuwa mchezaji muhimu katika kikosi cha Barcelona msimu huu lakini hatakuwepo katika mchezo huo baada ya Enrique kuamua kumpumzisha. Wakiwa bado na nafasi ya kupigania taji la La Liga, Ligi ya Mabingwa Ulaya na Kombe la Mfalme, kocha huyo amemua kutomuharakisha Vermaelen kurejea baada ya kupona majeruhi yaliyokuwa yakimkabili. Beki huyo wa kimataifa wa Ubelgiji hajacheza mechi yeyote ya mashindano kea Barcelona toka ajiunge nao akitokea Arsenal katika majira ya kiangazi mwaka jana baada ya kusumbuliwa na majeruhi ya misuli kwa kipindi kirefu. Wachezaji wengien walioachwa katika kikosi hicho in pamoja na Jordi Masip na Douglas, wakati Jordi Alba yeye ahatakuwepo kwasababu ya kutumikia adhabu.

No comments:

Post a Comment