Thursday, April 23, 2015

KUSHUHUDIA PAMBANO LA MAYWEATHER NA PAQUIAO MILIONI 18.

TIKETI kwa ajili ya pambano langumi la wiki ijayo kati ya bondia Floyd Mayweather na Manny Pacquiao hatimaye zinatarajiwa kuingia sokoni leo huku zikitegemwa kugharimu kiasi cha paundi 60,000. Ukumbi wa MGM Grand uliopo jijini Las Vegas, Nevada una uwezo wa kuingoza watazamaji 16,500 lakini in tiketi 1,000 pekee ndio zitakwenda sokoni. Tiketi zilizobakia zitakakwenda kwa mabondia wenyewe, casino, wadhamini na mapromota wa pambano hilo. Tiketi rahisi zaidi katika pambano hilo la Mei 2 mwaka huu zinatarajiwa kugharimu kiasi cha paundi 1,000 kwa pesa za madafu shilingi 2,903,000 na kupanda mpaka paundi 6,700 sawa na shilingi 18,869,500. Mayweather raia wa marekani ataingia katika pambano hilo akiwa na rekodi ya kushinda mapambano yake yote 47 ya kulipwa aliyocheza 26 kati ya hayo akishinda kea knockout wakati Pacquiao raia wa Filipino akiwa na rekodi ya kushinda mapambano 57, kupoteza matano na sare mawili.

No comments:

Post a Comment