Thursday, April 30, 2015

PARMA YASHUKA DARAJA RASMI.

KLABU ya Parma imeshuka rasmi kutoka katika Serie A baada ya msimu wa misukosuko ambao umewafanya kutangazwa mufilizi na kupokonywa alama tisa kutoka na makosa ya kifedha. Kipigo walichopata kutoka kea Lazio na sare ya mabao 2-2 dhidi ya Atalanta kinaifanya timu hiyo inayonolewa na Roberto Donadoni kukaa mkiani mwa msimamo wa ligi. Parma ilitangazwa mufilisi Machi mwaka huu wakiwa na deni linalofikia paundi milioni 54. Wachezaji wa timu hiyo hawajalipwa msimu huu na wamekuwa wakifua nguo zao wenyewe na kuendesha basi la timu. Parma ambao wamebadilisha wamiliki mara mbili msimu huu walikuwa washindi wa pili wa Serie A mwaka 1997 huku wakiwa wamewahi kushinda taji la Uefa Cup mwaka 1995 na 1999.

No comments:

Post a Comment