Tuesday, April 28, 2015

RAIS WA PSG AMKOMALIA CAVANI.

RAIS wa klabu ya Paris Saint-Germain, Nasser Al Khelaifi amasisitiza kuwa hataitazama ofa ya paundi milioni 50 kwa ajili ya Edinson Cavani kufuatia taarifa kuwa Manchester United itatoa kitita hicho kea ajili ya kuwania kumsajili. Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Uruguay amekuwa akihusishwa na tetesi za kwenda Old Trafford mara kadhaa lakini mabingwa hao wa Ufaransa wanaonekana kutokuwa na mpango wa kumuuza nyota huyo mwenye umri wa miaka 28 hivi karibuni. Akihojiwa Al Khelaifi amesema ameshafanya mazungumzo na Cavani kuhusiana na mustakabali wake hivyo ana uhakika kuwa ataendelea kuwa nao. Rais huyo alipoulizwa kuhusu ofa ya paundi milioni 50 iliyotolewa na United, alieleza kuwa hatataka hata kuitazama ofa kama hiyo.

No comments:

Post a Comment