Tuesday, April 28, 2015

YANGA KUKABIDHIWA NDOO YAO YA UBINGWA MEI 6 BAADA YA KUKIPIGA NA AZAM.

WAZIRI wa Habari, Vijana Utamuduni na Michezo, Dr. Fennela Mkangara anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika sherehe za kukabidhi Kombe la Ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom. Kwa mujibu wa taarifa kutoka Shirikisho la Soka nchini-TFF, Mkangara anatarajiwa kukabidhi kombe hilo kwa Yanga Mei 6, mwaka huu katika mchezo kati ya mabingwa hao dhidi ya Azam FC. Wakati huohuo rais wa TFF Jamal Malinzi ametuma salamu za pongezi kea mwenyekiti wa Yanga Yusufu Manji kufuatia timu huyo kutawadhwa mabingw wapya wa ligi hiyo. Katika salamu zake za pongezi, Malinzi amesema kutwaa Ubingwa wa VPL ni jambo muhimu na sasa wanapaswa kuanza maaandalizi kwa ajili ya michuano ya kimataifa barani Afrika mwakani . Yanga imetwaa ubingwa wa Ligi Kuu nchini kwa mara ya 25 jana, baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 4-1 dhidi ya timu ya Polisi Morogoro katika uwanja wa Taifa huku ikiwa na michezo miwili mikononi kabla ya ligi kumalizika.




No comments:

Post a Comment