Thursday, April 30, 2015

SPURS YAJIHAKIKISHIA KUNYAKUWA SCHNEIDERLIN.

KLABU ya Tottenham Hotspurs ina uhakika wa kushinda mbio za kumuwania nyota wa Southampton Morgan Schneiderlin katika kipindi hiki cha kiangazi huku wakiwa tayari kuwatoa nyota wake Andros Townsend au Benjamin Stambouli ili kusaidia kukamilisha azma hiyo. Klabu za Arsenal na Chelsea pia zimekuwa zikimuwinda nyota huyo wa kimataifa wa Ufaransa lakini Spurs sasa wanaamini lazima atatua White Hart Lane. Spurs walishajaribu kumsajili Schneiderlin majira ya kiangazi mwaka jana lakini ofa yao ilizuiwa na Southampton.Hata hivyo inaaminika kuwa sasa nyota huyo anataka kuondoka majira ya kiangazi huku Southampton wakiripotiwa kutaka kitita cha paundi milioni 20.

No comments:

Post a Comment