Thursday, April 23, 2015

WAKALA WA TOURE ADAI MTEJA HAJALI SANA FEDHA.

WAKALA wa Yaya Toure, Dimitri Seluk anatarajiwa kusimamisha mazungumzo na Manchester City baada ya kudai vilabu kadhaa vimejitokeza kutaka kumsajili kiungo huyo. Taarifa zinadai kuwa Toure amekuwa hana furaha katika klabu hiyo ambayo imeporomoka mpaka nafasi ya nne katika msimamo wa Ligi Kuu baada ya kupoteza mechi nne kati ya saba za mwisho walizocheza. Nyota huyo wa kimataifa wa Ivory Coast amekuwa akilaumiwakwa kucheza chini ya kiwango na kuigharimu timu yake jambo ambalo ndio linamfanya kufikiria mustakabali wake. Toure mwenye umri wa miaka 31 amebakisha miaka miwili katika mkataba wake wa sasa ambao unakadiriwa kuwa na thamani ya paundi milioni 10 kea mwaka lakini Seluk amerudia madai ya Toure kuwa pesa sio kigezo kinachoweza kugeuza maamuzi yake. Seluk amesema watu wengi wanadhani Toure atabakia kwasababu ya pesa lakini mwenyewe hajali kuhusu hilo.

No comments:

Post a Comment