Thursday, April 23, 2015

WENGER AKIRI KUCHEMKA KUMUUZA FABREGAS.

MENEJA wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger amekiri kujuta kumruhusu Cesc Fabregas kuondoka lakini amewataka mashabiki wa timu hiyo kumuheshimu kiungo huyo wa Chelsea pindi watakapocheza nao katika Uwanja wa Emirates Jumapili hii. Fabregas mwenye umri wa miaka 27 aliondoka Arsenal mwaka 2011 na kwenda Barcelona lakini baada ya kushindwa kupata nafasi ya kudumu katika kikosi cha kwanza alirejea katika Ligi Kuu kiangazi mwaka jana chini Jose Mourinho. Akihojiwa Wenger amesema kitu pekee anachojutia in kumuacha kiungo huyo aondoke lakini anachoataka yeye in kila mchezaji aheshimiwe. Meneja huyo aliendelea kudai kuwa anampongeza Fabregas kwa jinsi alivyoimarika na kuwa mchezaji tegemeo kwa Chelsea msimu huu.

No comments:

Post a Comment