Thursday, May 21, 2015

AMNESTY INTERNATIONAL YAITUHUMU QATAR KUENDELEA KUWANYANYAPAA WAFANYAKAZI.

SERIKALI ya Qatar imepinga madai ya shirika linalopigania haki za kibinadamu lenye makao yake nchini Marekani, Amnesty International, iliyodai kuwa maelfu ya wafanyakazi nchini humo wanaojenga viwanja vitakavyotumika katika michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2022 kuwa bado wanaonewa. Amnesty International ilikuwa imedai kuwa licha ya serikali hiyo kuahidi kuwalipa wafanyakazi mishahara yao kwa wakati unaofaa wengi bado hawapokei malipo yao kwa wakati unaostahili. Aidha Amnesty imelalamikia vikali mtindo wa Hawala ambao unamzuia mfanyakazi kuondoka nchini humo bila ruhusa ya mwajiri wake. Serikali ya Qatar imesema kuwa mabadiliko yanaendelea na kudai kuwa tayari mfumo wa kielektroniki ndio unaotumika kuwalipa wafanyakazi hatua inayohakikisha kuwa wanalipwa kwa wakati unaofaa. Hata hivyo Amnesty wanasema Qatar imepiga hatua kidogo sana kutekeleza ahadi nyingi walizozitoa mwaka jana, kwani wafanyakazi bado wanahitaji ruhusa kutoka kwa waajiri wao, kubadili ajira au kuondoka nchini humo huku malipo yao yakifanyika taratibu mno kea mfumo huo mpya.

No comments:

Post a Comment