Thursday, May 21, 2015

FABREGAS APUNGUZIWA ADHABU.

KIUNGO wa Chelsea, Cesc Fabregas amepunguziwa adhabu ya kufungiwa kutoka mechi tatu mpaka mechi moja baada ya kutolewa nje katika mchezo wa Ligi kuu dhidi ya West Bromwich Albion. Katika mchezo huo uliofanyika Jumatatu iliyopita, Fabregas alionyeshwa kadi nyekundu kwa kuonyesha kitendo kisicho cha uanamichezo wakati walipotandikwa mabao 3-0. Mwamuzi alimnyuka kadi hiyo baada ya Fabregas kupiga mpira uliompiga mchezaji wa West Brom kichwani wakati mchezo ukiwa umesimama. Katika taarifa iliyotolewa na klabu hiyo imedai kuwa adhabu hiyo imepunguzwa baada ya kuikatia rufani hivyo Fabregas atakosa mchezo wao mwisho wa msimu dhidi ya Sunderland.

No comments:

Post a Comment