Tuesday, May 19, 2015

CECH ANATAKA KWENDA ARSENAL, MAN UNITED AU PSG - WAKALA.

WAKALA wa golikipa wa Chelsea Petr Cech, amedai kuwa mteja wake angependelea kujiunga na klabu za Arsenal, Manchester United au Paris Saint-Germain katika usajili wa majira ya kiangazi. Cech ameshushwa mpaka kuwa golikipa namba mbili kutokana na ujio wa Thibaut Courtois katika klabu hiyo na wakala wake Viktor Kolar amebainisha awali kuwa mteja wake amepewa ruhusa ya kuondoka Stamford Bridge mwishoni mwa msimu. Arsenal wamekuwa wakihusishwa kwa muda mrefu na tetesi za kumtaka golikipa huyo wa kimataifa wa Jamhuri ya Czech, wakati United wao wanadhani Cech anafaa kuwa mbadala wa David De Gea kama akiondoka kwenda Real Madrid. Kolar amesema wanakarisha ofa kutoka timu hizo na kuongeza kuwa meneja wake Jose Mourinho hatakuwa na ushawishi wowote kuhusiana na mustakabali wake.

No comments:

Post a Comment