Tuesday, May 19, 2015

MOURINHO ATUPIA LAWAMA UPINZANI HAFIFU, KUFUATIA KIPIGO WALICHOPATA DHIDI YA WEST BROM.

MENEJA wa Chelsea, Jose Mourinho amewalaumu mahasimu wao katika Ligi Kuu kuwa ndio chanzo cha wao kutandikwa mabao 3-0 na West Bromwich Albion jana. Akihojiwa mara baada ya mchezo huo ambao kiungo wake Cesc Fabregas alitolewa nje kea kadi nyekundu dakika ya 29, Mourinho amesisitiza wachezaji wake wamepoteza ari baada ya kufanikiwa kunyakuwa taji. Kocha huyo aliendelea kudai kuwa wapinzani wao wakubwa Manchester City, Manchester United, Arsenal na Liverpool waliwaacha kushinda taji hilo mapema, hivyo kuwafanya kupoteza ile ari waliyokuwa nayo kabla. Mourinho amesema jambo hutokea kea timu nyingi akiifananisha Bayern Munich ambao nao wamepoteza michezo yao mitatu ya Bundesliga baada ya kunyakuwa taji hilo.

No comments:

Post a Comment