Tuesday, May 19, 2015

WENGER AMUWEKA STERLING KIPORO.

MENEJA wa Arsenal, Arsene Wenger amekataa kuweka wazi kama atatuma ofa kwa ajili ya kumuwania mshambuliaji wa Liverpool, Raheem Sterling. Mapema mwezi Aprili Sterling alibainisha nia ya Arsenal kumuhitaji, akifafanua kuwa ni heshima kubwa kwake, wakati Wenger akijibu kea kusisitiza hana nafasi ya kuleta mchezaji mpya katika kikosi chake. Akihojiwa kuhusiana na suala hilo Wenger amesema ni kweli watafanya usajili lakini kwasasa hataki kuzungumzia chochote kuhusiana na hilo kwani anaweza kudanganya. Kocha huyo aliendelea kudai kuwa kama akikubali kuwa atamuwania Sterling halafu asifanye hivyo kipindi cha usajili wanaweza kumuita muongo, hivyo ni vyema wakasubiri wakati muafaka wa kufanya hivyo.

No comments:

Post a Comment