Tuesday, May 19, 2015

BERLUSCONI KUMUONYESHA INZAGHI MLANGO WA KUTOKEA.

VYOMBO vya habari nchini Italia, vimeripoti kuwa Silvio Berlusconi amethibitisha kuwa atamtimua meneja wa AC Milan Filippo Inzaghi mwishoni mwa msimu baada ya matokeo yasiyoridhisha. Berlusconi ambaye ndiye mmiliki wa timu hiyo amesema Inzaghi amekuwa na mahusiano mazuri na kikosi chake lakini mara kadhaa wamekuwa wakipishana kutokana na maono tofauti. Bilionea huyo aliendela kudai kuwa jambo in kitu ambacho wanataka kuzungumza na kocha huyo muda ukifika kabla ya kuamua cha kufanya. Berlusconi amesema kwasasa wanajipanga na tayari wameshapata majina kadhaa ya makocha kama wakishindwa kufikia muafaka na Inzaghi.

No comments:

Post a Comment