Tuesday, May 19, 2015

QPR YAMPA MIAKA MITATU RAMSEY.

KLABU ya Queens Park Rangers-QPR, imeteua kocha wa muda Chris Ramsey(pichani) kuchukua kibarua cha moja kwa moja kuinoa timu hiyo kwa mkataba wa miaka mitatu. Ramsey mwenye umri wa miaka 53 alichukua mikoba hiyo kutoka kea Harry Redknapp Februari mwaka huu lakini alishindwa kuiwezesha timu hiyo kubakia katika Ligi Kuu.M Kocha huyo ambaye alikuwa mkuu wa zamani wa kitengo cha kukuza vipaji cha Tottenham hotspurs alijiunga na QPR Novemba mwaka 2014 kufuatia kuondoka kea Redknapp. QPR walishuka daraja kufuatia kutandikwa mabao 6-0 na Manchester City Mei 10 mwaka huu huku Ramsey akiwa amefanikiwa kupata ushindi kwenye mechi tatu kati ya 14 alizokuwa akiisimamia timu hiyo.

No comments:

Post a Comment