Tuesday, May 19, 2015

SOUTHAMPTON YATAKA PAUNDI MILIONI 25 KWA SCHNEIDERLIN.

KLABU ya Southampton inatarajia kutaka kitita cha paundi milioni 25 kwa ajili ya kiungo Morgan Schneiderlin(pichani) ambaye anawindwa na klabu za Arsenal na Tottenham Hotspurs. Klabu hizo zinazotoka kaskazini mwa jiji la London, zote zimeonyesha nia ya kumtaka kiungo huyo lakini Southampton wamedai hawatamuachia chini ya kiwango hicho. Southampton waligoma kupokea ofa yeyote kea ajili ya Schneiderlin kiangazi mwaka jana, wakati mchezaji huyo alipojaribu kulazimisha kuhamia Spurs. Klabu hiyo imepania kufanya kama usajili wa kiangazi mwaka jana ambapo walikunja kitita cha paundi milioni 25 kwa ajili ya Adam Lallana na paundi milioni 20 kwa Dejan Lovren ambao wote walikwenda Liverpool. Arsenal wamepanga kutuma ofa ya paundi milioni 20 kea ajili ya Schneiderlin wakati Spurs wao wako tayari kutoa kitita cha paundi milioni 15.

No comments:

Post a Comment