Monday, May 18, 2015

LUIS ENRIQUE HAENDI POPOTE - BARTOMEU.

RAIS wa Barcelona, Josep Bartomeu amesisitiza kuwa meneja wa Luis Enrique hataondoka katika timu hiyo mwishoni mwa msimu huu. Enrique alichukua mikoba ya Gerardo Martino aliyeondoka baada ya kushindwa kuipa mafanikio Barcelona msimu wa 2013-2014. Toka achukue mikoba ya kuinoa timu hiyo, Enrique amefanikiwa kubadilisha mambo na kuiwezesha timu hiyo kutwaa taji la La Liga msimu huu kufuatia kuifunga Atletico Madrid bao 1-0 jana. Tetesi zimezagaa kuwa kocha huyo anaweza kutimka kiangazi hiki lakini Bartomeu amekanusha vikali tetesi hizo na kudai ataendelea kubakia Camp Nou. Bartomeu amesema wako katika mazungumzo ya kumuongeza mkataba mpya hivyo hakuna shaka kuwa ataendelea kuwa nao.

No comments:

Post a Comment