Monday, May 18, 2015

VAN GAAL AKATA TAMAA KUMBAKISHA DE GEA.

MENEJA wa Manchester United, Louis van Gaal ameonyesha dalili za wazi za kumkosa golikipa wao David De Gea anayeweza kwenda Real Madrid. De Gea alitolewa nje baada ya kupata majeruhi msuli wakati wa mchezo dhidi ya Arsenal uliofanyika katika Uwanja wa Old Trafford jana hivyo kumfanya kuwa katika hatihati ya kuukosa mchezo wa mwisho dhidi ya Hull City. Madrid wamekuwa wakimuwinda kipa huyo wa kimataifa wa Hispania ili aweze kuchukua nafasi ya mkongwe Iker Casillas na Van Gaal ana uhakika De Gea anapata wakati mgumu kuchagua. Van Gaal amesema anajua sio rahisi kwa De Gea kuchagua kati ya klabu mbili kubwa, ingawa amedai watafurahi kama akibakia.

No comments:

Post a Comment