Tuesday, May 19, 2015

WATU 50 WAKAMATWA ITALIA KWA KOSA LA UPANGAJI MATOKEO.

ZAIDI wa watu 50 wamekamatwa na wengine kuwekwa chini ya upelelezi ikiwa in matokeo ya uchunguzi wa tuhuma za upangaji matokeo katika mechi za soka nchini Italia. Waendesha mashitaka wanaopambana na kundi haramu la Mafia katika mji wa Catanzaro uliopo kusini mwa Italia ndio walioongoza uchunguzi huo ambao umepeleka kukamatwa kwa watu hao. Kwa mujibu wa taarifa kutoka vyombo vya habari vya Italia, waliokamatwa in wachezaji 15, marais sita wa vilabu, maofisa nane wa michezo, makocha na viongozi 10 wa taasisi za kamari nchini humo. Uchunguzi huo uliohusisha polisi ilifanyika kwa kuzifuatilia mechi za ligi daraja la tatu, nne na tano ambazo ndio zimekuwa zikiongoza kwa tuhuma za upangaji matokeo. Mpango huo wa kupiga vita upangaji matokeo in mkakati wa kuliokoa soka la nchi hiyo ambalo lilikuwa limegubikwa na vitendo hivyo kuanzia timu za daraja la juu mpaka chini. Mwaka 2006 mabingwa wa sasa wa Serie A Juventus walishushwa daraja huku timu zingine zikikatwa alama baada ya kukutwa na hatia ya kuhonga waamuzi ili wawape upendeleo.

No comments:

Post a Comment