Tuesday, June 30, 2015

ARSENAL WAMPOKEA CECH KWA SHANGWE.

WACHEZAJI wa mbalimbali wa Arsenal wameungana na meneja wao Arsene Wenger kumkaribisha golikipa Petr Cech aliyetua Emirates akitokea kwa mabingwa wa Ligi Kuu Chelsea. Arsenal ilithibitisha jana kumsajili Cech kwa kitita ambacho kinaaminika kufikia paundi milioni 11. Nyota huyo anaondoka Chelsea baada ya kuitumikia kwa muda wa miaka 11 na kufanikiwa kushinda mataji mawili ya Ligi Kuu na Kombe la FA pamoja na moja la Ligi ya Mabingwa Ulaya. Wenger alimuelezea Cech kama mmoja wa magolikipa mahiri duniani na kuungwa mkono na wachezaji kadhaa wa timu hiyo ambao walitumia mitandao yao ya kijamii kumkaribisha. Miongoni mwa nyota walituma ujumbe wa kumkaribisha golikipa huyo katika kurasa zao za mitandao ya kijamii ni pamoja na Theo Walcott, Jack Wilshere, Aaron Ramsey, Olivier Giroud pamoja na golikipaWojciech Szczesny,

No comments:

Post a Comment