Tuesday, June 30, 2015

MAN UNITED YATOA OFA YA PAUNDI MILIONI 28.6 KWA AJILI YA KUMSAJILI RAMOS.

KLABU ya Manchester United imetuma ofa ya paundi milioni 28.6 kwenda Real Madrid kwa ajili ya kumsajili beki wake Sergio Ramos. United inaamini nyota huyo mwenye umri wa miaka 29 anataka kuondoka Madrid baada ya kushindwa kupewa ofa ya kuongezwa mkataba wake ambao unamalizika mwaka 2017. Nyota huyo wa kimataifa wa Hispania amecheza mechi 445 toka ajiunge na Madrid mwaka 2005 akitokea Sevilla. Meneja wa United Louis van Gaal anataka kuimarisha safu yake ya ulinzi katika kikosi chake tayari kwa ajili ya msimu ujao wa Ligi Kuu.

No comments:

Post a Comment