Tuesday, June 30, 2015

COPA AMERICA: VARGAS AIBUKA SHUJAA CHILE IKITINGA FAINALI.

WENYEJI Chile Alfajiri ya leo wamefanikiwa kutinga hatua ya fainali ya michuano ya Copa America baada ya kuigaragaza Peru kwa mabao 2-1 katika mchezo wa nusu fanali uliofanyika huko Santiago. Shujaa wa Chile katika mchezo huo alikuwa Eduardo Vargas ambaye alifinga mabao yote mawili katika dakika ya 42 na 64 na kumfanya kufikisha mabao 22 kwa nchi yake. Akihojiwa mara baada ya mchezo, Vargas ambaye anakipiga katika klabu ya Napoli ya Italia amesema alihisi mapema kuwa atafunga mabao katika mchezo huo kwani wakati wakifanya mazoezi Jumamosi alifunga karibu kila mpira aliopiga langoni. Chile sasa wanasubiri mshindi katika mchezo mwingine wa nusu fainali utakaochezwa baadae leo ambapo Argentina watakwaana na Paraguay.

No comments:

Post a Comment