Friday, June 26, 2015

BECKERNBAUER AMFUNDA GUARDIOLA.

NGULI wa soka wa Ujerumani, Franz Beckernbauer amemwambia meneja wa Bayern Munich Pep Guardiola kuwa anapaswa kushinda mataji kama anataka kuonyeshwa upendo. Mapema wiki hii Guardiola alibainisha kuwa moja na malengo yake makubwa katika maisha ni watu kumhusudu ya kutambua kazi yake na Beckernbauer amesisitiza kuwa mafanikio ni njia rahisi ya kukufanya upendwe na mashabiki. Nguli huyo amesema upendo ni jambo kubwa kwa mtu kupata na iwapo Guardiola anahitaji hilo njia rahisi ya kufanikisha in kuhakikisha anashinda mataji. Bayern imetawala Bundesliga chini ya Guardiola katika misimu miwili iliyopita kwa kushinda taji hilo kwa vipindi vyote hivyo lakini Beckernbauer anadhani kocha huyo atakabiliwa na wakati mgumu kuhakikisha anatetea taji hilo msimu ujao.

No comments:

Post a Comment