Friday, June 26, 2015

BLATTER ADAI HAJAJIUZULU.

RAIS wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA Sepp Blatter amesema hajajiuzulu nafasi yake hiyo katika shirikisho hilo. Blatter mwenye umri wa miaka 79 alikuwa akifikiriwa kuwa amejiuzulu nafasi hiyo ambayo ameiongoza kwa kipindi cha miaka 17 kufuatia madai ya ufisadi yaliyoikumba shirikisho hilo. Lakini kwa mujibu wa gazeti la Blick, Blatter alikaririwa akidai kuwa hajajizulu bali ameacha mustakabali wake uamuliwe katika Mkutano Mkuu wa FIFA. Kauli hiyo imezusha hofu kuwa Blatter anafikiria kugombea tena nafasi hiyo katika uchaguzi mwingine.

No comments:

Post a Comment