Thursday, June 25, 2015

LAPORTA AAHIDI KUMSAJILI POGBA AKICHAGULIWA KUIONGOZA TENA BARCELONA.

MGOMBEA urais wa klabu ya Barcelona, Joan Laporta ana uhakika kiungo wa Juventus Paul Pogba atakuwa radhi kutua Camp Nou. Nyota huyo wa kimataifa wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 22, amekuwa akitajwa kama mmoja wachezaji bora kabisa katika soka kipindi hiki na amekuwa kihusishwa na tetesi za kuondoka jijini Turin zaidi ya mara moja pamoja na kuwa na mkataba na mabingwa hao wa Serie A mpaka mwaka 2019. Barcelona in moja wapo ya timu zilizoonyesha in ya kumsajili Pogba na Laporta amedokeza yuko tayari kumsajili kiungo huyo kama akichaguliwa kuwa rais wa klabu hiyo tena. Laporta alijinadi kuwa amekuwa na mahusiano ya karibu na wakala wa mchezaji huyo Mino Raiola hivyo anaamini haitamuwia vigumu kumsajili mchezaji huyo kama kichaguliwa tena kuiongoa timu hiyo. Laporta ambaye amewahi kuingoza Barcelona kuanzia mwaka 2003 mpaka 2010 anakabiliwa na upinzani kutoka kwa rais wa sasa Josep Maria Bartomeu, Jordi Majo na Agusto Benedito katika uchaguzi huo unaotarajiwa kufanyika mapema mwezi ujao.V

No comments:

Post a Comment