Thursday, June 25, 2015

SOUTHGATE AKOMAA PAMOJA NA KUTOLEWA EURO U21.

KOCHA wa timu ya taifa ya Uingereza kwa vijana chini ya umri wa miaka 21, Gareth Southgate amedai kuwa bado anataka kuendelea kuinoa timu hiyo pamoja na kuenguliwa katika michuano ya Ulaya kwa vijana wa umri huo inayoendelea huko Jamhuri ya Czech. Uingereza jana ilishindwa kufua dafu mbele ya Italia baada ya kukubali kucharangwa mabao 3-1 katika mchezo huo. Southgate ambaye mkataba wake unafikia kikomo mwaka 2017 amesema anataka kuendelea mpaka hapo atakapomaliza mkataba huo. Southgate alikwenda katika michuano hiyo ya nyota Saido Berahino aliyekua majeruhi, huku akiwakosa Raheem Sterling, Jack Wilshere na Ross Barkley ambao wangeweza kukisaidia kikosi hicho lakini waliachwa kutokana na majukumu yao katika timu ya wakubwa.

No comments:

Post a Comment