Thursday, June 25, 2015

WENGER AANZA USAJILI KATIKA MAFUNGU, BAADA YA KUMSAJILI KINDA WA ROMANIA KWA EURO 100,000.

KLABU ya Arsenal imekamilisha usajili wa Vlad Dragomir kutoka klabu ya ACS Poli Timisoara kwa ada ya euro 100,000 huku kiungo huyo chipukizi akiepwa mkataba wa miaka mitatu. Usajili wa Dragomir mwenye umri wa miaka 16 unakuwa wa kwanza kufanyika katika kipindi hiki cha kiangazi na anatarajiwa kujiunga na akademi ya klabu hiyo. Chipukizi huyo ambaye alikuwa nahodha wa kikosi cha timu ya taifa ya Romania kea vijana chini ya umri wa miaka 16, alikuwa akihusishwa na tetesi za kwenda Inter Milan lakini mwenyewe amekiri nafasi ya kujiunga na Arsenal waliyopata ilikuwa ngumu kuikataa. Akihojiwa Dragomir amesema ofa aliyopewa na Arsenal ilionekana kuwa bora kwake na amefurahi kukamilisha usajili huo.

No comments:

Post a Comment