Monday, July 27, 2015

ASTON VILLA YAKARIBIA KUMNASA CRESPO.

KLABU ya Cordoba imebanisha kuwa beki Jose Angel Crespo anatarajiwa kufanyiwa vipimo vya afya Aston Villa baada ya klabu hizo mbili kufikia makubaliano kuhusu ada ya uhamisho wake. Beki huyo mwenye umri wa miaka 28 msimu uliopita alikuwa akicheza kwa mkopo katika klabu ya Andalusian. Cordoba ambayo ilishuka daraja msimu uliopita baada ya kumaliza wa mwisho katika msimamo wa La Liga, wamedai leo kuwa Crespo anakaribia kukamilisha uhamisho wake kwenda Villa Park. Taarifa hizo zilithibitishwa katika mtandao wa klabu hiyo na kudai kuwa tayari beki huyo amesafiri kuelekea nchini Uingereza kwa ajili ya vipimo vya afya.

No comments:

Post a Comment