Thursday, July 23, 2015

ATLETICO YANASA SAINI YA NYOTA WA GHANA.

KLABU ya Atletico Madrid imekubali kumsajili kiungo wa kimataifa wa Ghana Bernard Mensah kutoka klabu ya Vitoria Guimaraes ya Ureno. Hata hivyo, Atletico watampeleka kiungo huyo kwa mahasimu wao wa La Liga na majirani zao Getafe. Klabu hiyo ilithibitisha tarifa hizo kupitia mtandao wake jana huku wakidai kumpeleka kwa mkopo wa msimu mmoja Getafe. Vitoria na Getafe pia zilithibitisha dili hilo la nyota huyo mwenye umri wa miaka 20 ambaye ambali na kucheza kama kiungo wa kushambulia lakini pia anaweza kucheza kama winga.

No comments:

Post a Comment