Thursday, July 23, 2015

BENTEKE TO LIVERPOOL DONE DEAL.

LIVERPOOL imefanikiwa kumsajili rasmi mshambuliaji wa Aston Villa, Christian Benteke kwa kitita cha paundi milioni 32.5. Benteke anakuwa mchezaji wa pili ghali kusajiliwa na Liverpool. Liverpool ambao wiki iliyopita walimuuza mshambuliaji Raheem Sterling kwenda Manchester City kwa kitita cha paundi milioni 49, walifanikiwa kunasa saini ya Benteke na kumfanya kuwa mchezaji wa saba kusajiliwa na timu hiyo kipindi hiki cha kiangazi. Nyota huyo wa kimataifa wa Ubelgiji amefunga mabao 49 katika mechi 101 alizoichezea Villa baada ya kumsajiliwa kutoka Genk kwa kitita cha paundi milioni saba mwaka 2012. Akihojiwa mara baada ya kukamilisha usajili huo Benteke alieleza kufurahishwa kwake na hatua hiyo na kuahidi kufanya kila awezalo kuhakikisha mataji yanamiminika Anfield.

No comments:

Post a Comment