Thursday, July 23, 2015

BAYERN YAIAMBIA UNITED ILIE TU KWA MULLER.

OFISA mkuu wa Bayern Munich, Karl-Heinz Rummenigge amewaonya Manchester United kuwa hakunja fedha zitakazotosha kwa ajili ya wao kumsajili Thomas Muller. United iliyo chini Louis van Gaal tayari imeshamsajili Bastian Schweinsteiger kutoka kwa mabingwa hao wa Bundesliga mapema mwezi huu na tetesi ziliibuka kuwa wako tayari tena kutoa ofa ya euro milioni 100 kwa ajili ya Muller. Akihojiwa na wanahabari katika ziara yao nchini China, Rummenigge amesema kuna wachezaji hawauziki kwa gharama yeyote na mmojawapo nia Muller. Rummenigge aliendelea kudai kuwa hawajawahi kupokea simu yeyote kutoka United na hakuna ofa iliyotolewa na yeyote kwa ajili ya mchezaji huyo.

No comments:

Post a Comment