Saturday, July 18, 2015

GERRARD ATUPIA KATIKA GEMU LAKE LA KWANZA MLS.

NAHODHA wa zamani wa kimataifa wa Uingereza na klabu ya Liverpool, Steven Gerrard amefanikiwa kufunga bao lake la kwanza katika Ligi Kuu nchini Marekani huku akisaidia mengine mawili kati ya matatu yaliyofungwa na Robbie Keane wakati Los Angeles Galaxy ikiibatua San Jose Earthquakes. Mkongwe huyo mwenye umri wa miaka 35, alifunga bao lake hilo katika dakika ya 37 ya mchezo katika ushindi wa mabao 5-2 walioupata. Huo ndio ulikuwa mchezo wa kwanza wa kimashindano aliocheza Gerrard katika timu hiyo toka ajiunge nao mapema mwezi huu akitokea Liverpool. Sasa anakuwa mchezaji wa tatu kufunga bao, kusaidia moja na kusababisha penati katika ligi hiyo msimu huu, huku wengine wakiwa nyota wa zamani wa Serie A Sebastian Gionvico na Kaka.

No comments:

Post a Comment