Saturday, July 18, 2015

JUVENTUS WARUDIA KWA FERUFI KUBWA KUWA POGBA HAUZWI.

KLABU ya Juventus imeongeza msisitiza kiungo wake Paul Pogba hatauzwa, pamoja na kutolewa kwa ofa na klabu ya Barcelona. Joan Laporta amedai kuwa ataweza kumsajili nyota huyo mwenye umri wa miaka 22, ambaye pia amehusishwa na tetesi za kutakiw Manchester City na Chelsea, kama akichaguliwa kuwa rais wa Barcelona tena. Mkuruzenzi wa Juventus Giuseppe Marotta amesema yeyote anayamtaka mchezaji huyo anapswa kuzungumza nao na sio kwenda kwa wakala wake Mino Raiola. Marotta aliendelea kudai kuwa kwasasa Barcelona hawazi kufanya usajili wowote na Juventus hawana mpango wa kumuuza Pogba. Nyota huyo wa kimataifa wa Ufaransa ambaye amewahi kuwa mchezaji wa Manchester United, ana mkataba na Juventus ambao unamalizika Juni mwaka 2019.

No comments:

Post a Comment