Saturday, July 18, 2015

MAN UNITED YAIBANA MADRID, YAWAAMBIA BILA RAMOS HAWAMPATI DE GEA.

KLABU ya Manchester United wanajiandaa kupoteza zaidi ya paundi milioni 25 na kumuacha golikipa wao David De Gea kuondoka kama mchezaji huru majira ya kiangazi mwakani kuliko kuwauzia Real Madrid. Golikipa huyo mwenye umri wa miaka 24, atauzwa pale tu Madrid watakapokubali kumuachia beki wao Sergio Ramos mwenye umri wa miaka 29 kwenda United. De Gea ambaye amekuwa katika mipango ya Madrid kipindi hiki cha kiangazi, amebakisha mkataba wa mwaka mmoja na anataka kurejea nyumbani. Lakini United wameamua kukomaa na golikipa huyo hata kama ataodoka bure mwakani ili waweze kutoa msukumo kwa Madrid kumuachia Ramos.

No comments:

Post a Comment