Tuesday, September 29, 2015

BARCELONA WAPATA TAARIFA NJEMA KWA ALBA.

KLABU ya Barcelona imepata ahueni baada ya Jordi Alba kuruhusiwa kucheza katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Bayer Leverkusen ya Ujerumani kesho. Klabu hiyo tayari itawakosa Adriano ambaye anasumbuliwa na majeruhi msuli huku nyota wao Lionel Messi akitarajiwa kukaa nje kwa kipindi cha wiki nane baada ya kupata majeruhi ya goti Jumamosi iliyopita. Rafinha, Thomas Vermaelan na Claudio Bravo ni wachezaji wengine ambao watakosekana katika mchezo huo wa pili wa hatua za makundi ya michuano hiyo. Katika mchezo wa kwanza Barcelona waliambulia sare ya bao 1-1 dhidi ya AS Roma ya Italia, mchezo uliofanyika katika Uwanja wa Olimpico.

No comments:

Post a Comment