Tuesday, September 29, 2015

MOURINHO ADAI COSTA ANAONEWA.

MENEJA wa Chelsea Jose Mourinho amedai mshambuliaji wake Diego Costa amekuwa akionewa na maafisa wasimamizi wa soka. Akiongea na wanahabari kuhusu mechi ya leo dhidi ya klabu yake ya zamani ya FC Porto ya Ureno katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya, Mourinho amesema waamuzi wamekuwa na hamu kubwa na kumsimamisha mshambuliaji huyo. Costa amefungiwa kutocheza mechi tatu na Shirikisho la Soka la Uingereza-FA baada ya kupatikana na hatia ya utovu wa nidhamu wakati wa mechi ya Ligi Kuu dhidi ya Arsenal. Lakini yuko huru kucheza dhidi ya Porto leo kwani adhabu hiyo hiyo haigusi mechi za Ulaya.

No comments:

Post a Comment