Tuesday, September 29, 2015

ROONEY AMZODOA FERGUSON.

NAHODHA wa Manchester United, Wayne Rooney amekanusha kupeleka ombi la kutaka kuondoka mwaka 2013 katika kipindi chake kipya cha kusherekea mafanikio yake nchini Uingereza. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 29, ambaye hivi karibuni amekuwa mfungaji bora wa wakati wote, amekuwa akivumilia mahusiano ya misukosuko na meneja wa zamani wa United Sir Alex Ferguson, na kuomba kuondoka mwaka 2010 kabla ya kupewa mkataba mpya. Wawili hao walikwaruzana tena miaka mitatu baadae wakati wa msimu wa mwisho wa Ferguson wakati Rooney alipojikuta akitengwa katika kikosi cha meneja huyo. Katika mchezo wake wa mwisho Old Trafford Ferguson alidai kuwa, mshambuliaji huyo aliomba kuondoka tena lakini Rooney mwenye anakanusha vikali kwa kueleza hali halisi ilivyokuwa. Rooney amesema alimfuata Ferguson na kumwambia kuwa kama hatakuwa akimchezesha ni bora akaondoka zake lakini anashangaa haraka jambo hilo lilidakwa na vyombo vya habari na kupotoshwa jambo ambalo halikuwa kweli.

No comments:

Post a Comment